Lyrics

Pusha washa mi nina stress zimejaa kwenye kichwa
Sogeza kiti kaa nikueleze machache yaliyonikuta
Kuna kijanaa ananisumbua sanaa
Mke wangu raha hana, nyumbani amani hakuna hi hii
Asidhani mimi ni mkimya sana, mwenzie naumia roho yangu
Nisije baadae mi kupata lawama, nikaharibu CV yangu
(Mwambieni) Ama zake ama zangu mi ntakufa naye
(Nasema mwambieni) Ama zake ama zangu mi nitakufa naye
(Mkimuona mwambieni) Ama zake ama zangu nitakufa naye
(Eeh mwambieni) Ama zake ama zangu nitakufa naye
Anapitaga kibarazani, nguo kashusha makalioni
Anajifanya yeye muhuni, wenzie tulianza tisini
Tutabadilishana majengo ya serikali
Mi niende jela, yeye aende mochwali
Asidhani mimi ni mkimya sana, mwenzie naumia roho yangu
Nisije baadae mi kupata lawama, nikaharibu CV yangu
(Mwambieni) Ama zake ama zangu mi ntakufa naye
(Nasema mwambieni) Ama zake ama zangu mi nitakufa naye
(Mkimuona mwambieni) Ama zake ama zangu nitakufa naye
(Eeh mwambieni) Ama zake ama zangu nitakufa naye
Haiyo, haiyo, haiyoyo
Huwaga sipendagi dharau
Haiyo, haiyo, haiyoyo
Mwambie anajisahau
Haiyo, haiyo, haiyoyo
Tutachukiana mamaa
Haiyo, haiyo, haiyoyo
Tutapeana lawana sana
Written by: Aslay Isihaka Nassoro
instagramSharePathic_arrow_out