Lyrics

[Verse 1]
Ndo kusema kwamba nina bahati mbaya
Ama ni nyota imefifia ah
Maana sio kweli
Kila siku mimi ndo naumia
[Verse 2]
Ndo kusema kwamba sura yangu mbaya
Haina hulka ya kuvutia ah
Maana sio kweli
Kila siku mimi ndo naumia
[Verse 3]
Ina maana penzi ningekuwa chombo cha usafiri
Ningekosa hata sehemu ya kusimama
Ningewezaje? Nitawezaje?
[Verse 4]
Au labda mapenzi hufaa kwa matajiri
Alafu mi hapa sina maana
Sa nitaanzaje? Nitaanzaaje?
[Verse 5]
Inawezekanaje nikose kufurahi
Siku zote ninazoishi na uhai
Najua Mungu hapendi
Walimwengu mna visa
[PreChorus]
Nikisema niage nitakuwa najilaghai
Moyo utakuwa bado unanidai
Acha niweke imani
Ipo siku nitaridhishwa
[Chorus]
Aya!
Aya!
Aya!
Aya!
[Verse 6]
Na sinacho maanisha mnakijua
Kuyakosa mapenzi inanitesa
Sawa nakua nayaona
Sa mbona yananizidia?
[Verse 7]
Hivi nacho maanisha mnakijua?
Upweke unanitesa
Halafu nakuwa nawaona
Wengine wanaenjoy (Aah!)
[Verse 8]
Ingekuwa gambe ndio dawa ya mawazo
Ningekunywa nilewe
Aah nilewe, nilewe
[Verse 9]
Inawezekanaje nikose kufurahi
Siku zote ninazoishi na uhai
Najua Mungu hapendi
Walimwengu mna visa
[PreChorus]
Nikisema niage nitakuwa najilaghai
Moyo utakuwa bado unanidai
Acha niweke imani
Ipo siku nitaridhishwa
[Chorus]
Aya!
Aya!
Aya!
Aya!
Written by: Omary Ally
instagramSharePathic_arrow_out