Featured In

Credits

PERFORMING ARTISTS
Upendo Nkone
Upendo Nkone
Performer
COMPOSITION & LYRICS
Upendo Nkone
Upendo Nkone
Songwriter

Lyrics

Hapa nilipo ni kwa neema yako tu
Nimefika ni kwa nguvu zako tu
Nilipo toka ni mbali sanaa
Milima na mabonde nimepita mimi
Hapa nilipo ni kwa mkono wako tu
Nimefikaa, ni kwa uweza wako tuu
Umenishika mkono Yesu! Nashukuru Bwana!
Mi nashukuru, nashukuru Yesu, nashukuru
Wakati mwingine nilizungukwa na magonjwa, tabu nyingi
Na uchumi kudidimia, nikapata mateso sanaa!
Nilizidi kukufuata Yesuu
Kwa macho yako ya huruma na upendo ukaniona ukasema nisiogope
Ukanitia nguvu Yesu! Ukasema nijipe moyo wewe uko nami
Nashukuru Yesu, mimi nashukuru
Pamoja na mambo mengi niliyopitia mimi-mimi
Pamoja na mengi ninayopitia sasa
Pamoja na ujane nilionao mimi hee!
Sitaogopaa! Sitaogopaa! Sitaogopaa!
Najipa moyo mimi (Najipa moyo), moyo (Siku moja nitafika)
Safari yangu mimi (Safari yangu mi najua nitafika tu), safari yangu
Naomba uniongozee Bwana (Najipa moyo siku moja nitafika) uniongozee Bwana
Unilinde na mabaya yote Baba (Safari yangu ni najua nitafika tu)
Kwa kuwa Yesu ni kiongozi wa safari yangu mimi (Najipa moyo siku moja nitafika)
Wakati huu nikiwa ni mjane nakutazama, unifariji moyo wangu
Bila wewe mimi siwezi, nikiwa na wewe nitashinda
Ninakuomba uwalinde wajane wote na uwatunze na yatima nao wakutazama
Shughulika na shida zao, Yesu
Uwapiganie Baba ndiwe tegemeo na uwatetee! Ee Yesu!
Najipa moyo (Najipa moyo siku moja nitafika)
Nanyenyekea kwako Yesu (Safari yangu), niongoze Baba (Mi najua nitafika tu)
Naomba unishike kwa mkono wako (Najipa moyo siku moja nitafika)
Naomba unilinde mie Baba (Safari Yangu mi najua nitafika tu)
Nakuamini Yesu
Kwa kuwa Yesu ni kiongozi wa safari yangu mimi ooh! (Najipa moyo siku moja nitafika)
Mi bado najipa moyoo! (Najipa moyo siku moja nitafika) sijakata tamaa
Ninavumumilia mambo yotee shida na tabu (Safari yangu ninajua nitafika tu)
Mi bado najipa moyo (Najipa moyo siku moja nitafika)
Bado navumilia shida (Safari yangu mi najua nitafika) najuaa
Utanioshaa Bwanaa
Kwa kuwa Yesu ndiye mlinzi wa safari yangu mimi yeye (Najipa moyo siku moja nitafiikaa)
Written by: Upendo Nkone
instagramSharePathic_arrow_out